Kwa mujibu wa shirika la habari la Abna, Volodymyr Zelenskyy, katika ujumbe wake wa video wa usiku, akirejelea kupokea ripoti ya uwanjani kutoka kwa Oleksandr Syrskyi, Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Silaha vya Ukraine, alisema: "Pande za Pokrovsk, Lyman na maeneo mengine katika Mkoa wa Donetsk, pamoja na maeneo ya mpakani katika Mikoa ya Sumy na Kharkiv, zinakabiliwa na hali ngumu."
Aliwataka raia wa Ukraine kuzingatia kwa uangalifu maonyo ya mashambulizi ya anga katika siku zijazo na kusisitiza kwamba matokewa ya mwisho ya vita yanategemea upinzani wa vikosi vya ulinzi na usalama vya Ukraine na juhudi za pamoja za kuihifadhi nchi hiyo.
Your Comment